Posts

Showing posts from May, 2022

MIAKA MIWILI TANGU KIFO CHA GEORGE FLOYD: Namna kifo chake kilivyomfanya kuwa alama ya mapambano dhidi ya mauwaji na ubaguzi wa rangi.

Mei 25, 2020, miaka miwili iliyopita, majira ya saa mbili usiku George Perry Floyd Jnr, alinunua pakiti la sigara katika duka linaloitwa Cup Foods katika makutano ya mtaa wa 38 wa Mashariki na mtaa wa Chicago kule Minneapolis, Marekani. Mwajiriwa wa duka lile alimshutumu Floyd kuwa alinunua pakiti lile la sigara kwa noti feki ya $20 na kuamua kumripoti. Baada ya maafisa wa polisi kufika eneo la tukio, walimtia mbaroni Bw. Floyd na kuifunga mikono yake nyuma kwa pingu, kumsogeza kando ya gari lao walipomlaza chini kabla ya afisa mmoja kuamua kumkandamiza shingoni kwa kutumia goti lake mpaka mauti ilipomfika. George Floyd ni moja kati ya mamia, pengine maelfu ya watu waliouwawa kikatili kutokana na ubaguzi wa rangi (racism and white supremacy). Tofauti kubwa ni kwamba, muhanga wa safari hii katika mauwaji ya kikatili yanayosababishwa na dhana za kibaguzi, aliuwawa kikatili huku video iliyoonyesha mauwaji hayo kuanzia alipokamatwa mpaka kifo chake ikizua hisia za huzuni na mshtuko kwa w...

Ugonjwa wa 'Monkeypox': Je, tunapaswa kuwa na wasiwasi?

‘Monkeypox’ ni ugonjwa unaosababishwa na kirusi ambacho hutoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu (kitaalamu huitwa ‘viral zoonosis’). Huu ni ugonjwa wenye dalili zinazofanana na zile zilizokuwa zikionekana kwa wagonjwa wa ndui (smallpox), licha ya kuwa madhara yake mwilini sio makali kama yale ya ndui. Monkeypox kimsingi ni ugonjwa ambao umekuwepo katika Afrika ya Kati na Magharibi, sanasana katika maeneo ya misitu ya mvua ya kitropiki na umekuwa ukisambaa kuelekea maeneo ya mijini. Jamii kadhaa za wanyama zimetajwa kuathirika zaidi na kirusi cha ugonjwa huu wa ‘Monkeypox’ ikiwemo aina fulani ya nyani, jamii za chindi (squirrels), panya kutoka Gambia, na aina zingine kadhaa za wanyama. Kisa cha kwanza cha Monkeypox kiliripotiwa mwaka 1970 katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kwa mvulana wa miaka tisa katika kipindi ambacho harakati nyingi sana za kupambana na ugonjwa wa ndui zilikuwa zikiendelea huku visa zaidi vikiendelea kuripotiwa Afrika ya Kati Pamoja na Afrika Magharibi. Tang...

COVID-19: A Sanguine Prediction of the 'New Normal'

  “WHO has been assessing this outbreak around the clock and we are deeply concerned both by the alarming levels of spread and severity, and by the alarming levels of inaction.” These words were said by the WHO director-general, Dr. Tedros Adhanom Ghebreyesus at a media briefing on COVID-19 on March 11 th 2020. “We have therefore made the assessment that COVID-19 can be characterized as a pandemic.” he added. COVID-19 pandemic is an ongoing global pandemic of coronavirus disease 2019 caused by Severe Acute Respiratory Syndrome Coronavirus 2 (SARS-CoV-2). The novel virus was identified vfrom an outbreak in Wuhan, China, a city with over 11 million people in December 2019 as a strange new pneumonia. On January 30 th 2020, the outbreak of COVID-19 was declared a Public Health Emergency of International Concern (PHEIC) by the WHO. Globally, as of 5:22pm CEST, 25 th April 2022, there had been 507,501,771 confirmed cases of COVID-19, including 6,220,390 deaths reported to WHO [All acc...

MFUMUKO WA BEI YA MAFUTA: Namna vita ya Urusi na Ukraine inavyochangia kupanda kwa bei ya mafuta na hatua zinazochukuliwa na serikali kukabiliana na mfumuko huo nchini Tanzania.

Moja kati ya mijadala mizito iliyozuka mitandaoni katika siku za hivi karibuni ni suala la kupanda kwa bei ya mafuta hadi kufikiwa kiwango cha juu zaidi kuwahi kuwepo katika soko la dunia kwa takribani miaka 14 sasa. Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Mei 3 mwaka huu ilitangaza bei mpya kikomo za bidhaa za mafuta ya petroli kutumika kuanzia Mei 4 hapa nchini. Huku hali ya taharuki ikizuka kutokana na bei hizo kuwa juu sana mfano, bei elekezi ya mafuta ya petroli kwa rejareja jijini Dar-es-salaam ikiwa ni Tsh.3,148/= na bei ya dizeli ikiwa ni Tsh.3,264/=, serikali imekwisha toa tamko bungeni juu ya hatua za dharura zitakazochukuliwa. Aidha, watu wengi wamekuwa wakihoji uwiano na uhusiano wa kupanda kwa bei ya mafuta na sababu kubwa inayoelezwa kuwa ndiyo chanzo; vita ya Urusi na Ukraine. Ni kwa vipi vita ya Urusi na Ukraine inapelekea mfumuko wa bei ya mafuta? Mnamo Februari 24 mwaka huu, nchi ya Urusi iliivamia na kuingia ndani ya mipaka ya nchi ya Ukraine kat...